IQNA

Siku ya Kimataifa ya Quds mjini Tehran

12:39 - May 08, 2021
Habari ID: 3473888
TEHRAN (IQNA)- Wakaazi wa Tehran, mji mkuu wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran wameshiriki katika mijumuiko isiyo rasmi Ijumaa katika Siku ya Kimataifa ya Quds kwa lengo la kubainisha uungaji mkono wao kwa Wapalestina na kulaani utawala haramu wa Israel.

Mijumuiko huyo aghalabu ilikuwa misafra ya magari na pikipiki ambapo bendera za Palestina zimepeperushwa huku bendera za Marekani na Israel zikikanyagwa au kuteketezwa moto.

 
 
captcha