IQNA

Muungano wa kimataifa dhidi ya ISIS ni dharura

16:00 - September 16, 2015
Habari ID: 3363344
Mjumbe maalumu wa Umoja wa Mataifa Nickolay Mladenov Mashariki ya Kati amesema kunahitajika muungano wa kimatiafa wa kijeshi ili kuangamiza kundi la kigaidi la ISIS au Daesh.

Katika mahojiano na televisheni ya BNT Nickolay Mladenov amesmea kundi la kigaidi na kitakfiri la ISIS haliwezi kuangamizwa pasina kuwepo muungano wa kimataifa wa kijeshi.
Akiashiria hali ya mambo nchini Syria amesema: "Udiplomasia na maamuzi ya kisiasa ndio njia pekee inayofaa kumaliza mapigano katika nchi hii inayokumbwa na vita."
Nickolay Mladenov aidha amegusia hali ya mambo ya wakimbizi Waislamu na sera za baadhi ya nchi kuhusu suala hilo na kusema: "Zinapaswa kuchukuliwa hatua ili wahamiaji wapewe hifadhi katika maeneo yaliyo karibu na nchi zao ili hali ikiboreka warejee haraka."
Mladenov pia ametoa wito kwa nchi za Ulaya kutenganisha baina ya wakimbizi wanaokimbia vita na wale wanaotafuta ajira katika bara hilo.../mh

3363182

captcha