Nakala hizo za Qur'ani ziki katika kifurushi kilichopewa jina la, 'Basirah Mushaf', na zimechapishwa kwa ushirikiano wa shirika moja la Malayasia.
Qur'ani hiyo yenye hati ya Braille pia ina kalamu ya kielektroniki yenye kuzungumza ambayo inawawezesha watumizi kuchagua na kusikiliza aya za Qur'ani. Aidha kifurushi hicho kinajumuisha pia qiraa ya wasomaji mashuhuri wa Qur'ani, maana ya ibara za Qur'ani, sababu za kuteremka sura n.k.
Tokea mwaka 2014, taasisi hiyo imesambaza nakala 6000 za Qur'ani Tukufu zenye hati za Braile kwa ajili ya wenye ulemavu wa machi katika mabara ya Asia, Afrika na Ulaya.
Nakala hizo maalumu za Qur'ani zenye hati ya Braille zimesambazwa Oktoba 15 kwa munasaba wa Siku ya Walemavu wa Macho.