Wizara ya Hijja na Umrah ya Saudi ilitangaza ufunguzi wa usajili siku ya Jumapili.
Wale wanaotaka kuhiji kutoka kwa Ufalme wanaweza kujiandikisha kupitia tovuti ya wizara localhaj.haj.gov.sa au kupitia programu ya Nusuk kwenye simu ya mkononi au kompyuta kuanzia saa moja jioni Jumapili, Februari 11.
Huko wanaweza kukagua chaguo vifurishi mbali mbali vya Hija, huku uhifadhi ukipewa kipaumbele kwa wale ambao hawajawahi kuhiji hapo awali.
Ili kurahisisha usajili, wizara imewezesha ama kulipa kiasi chote baada ya usajili au kulipa kiasi fulani kulingana na sheria na masharti yaliyotajwa.
Wizara iliwataka waliojiandikisha kuhakikisha usahihi wa taarifa wakati wa kusajili na kuchagua vifurushi, ikisisitiza umuhimu wa kutotumia nambari moja ya simu kwa zaidi ya programu moja.
Maswali yanaweza kutumwa kwa wizara kupitia barua pepe kwa care@haj.gov.sa, kwa kupiga simu kwa Kituo cha Huduma ya Mahujaji kupitia 1966 kutoka ndani ya Ufalme au kupiga nambari 920002814 - kutoka ndani na nje ya Ufalme, au kupitia kwenye X: @MOHU_Care.
Hija ni safari ya kwenda Makka ambayo kila Mwislamu mwenye uwezo wa kimwili na uwezo wa kifedha analazimika kuitimiza angalau mara moja katika maisha yake.
Takriban Waislamu milioni 2.5 kutoka sehemu mbalimbali za dunia hushiriki katika ibada ya Hija kila mwaka.
3487160